Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu
(Simiyurrh)

MAFUNZO YA WATUMISHI WAPYA (INDUCTION COURSE) TOKA MKAPA FOUNDATION

Posted on: May 15th, 2020

Serikali imeweka kipaumbele katika kuwajengea uwezo Watumishi wake ili kutimiza majukumu yao kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuongeza nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa umma. Hayo yamesemwa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu, Dr Matoke Muyenjwa alipokuwa akifungua mafunzo kwa waajiriwa wapya  17 toka Shirika la Mkapa Foundation

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Simiyu, Dr Matoke Muyenjwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya watumishi  wapya toka Mkapa Foundation katika ukumbi wa mikutano wa Hopsitali 

Kiongozi huyo amesema utoaji wa mafunzo hayo  utasaidia kutoa maarifa mapya, ujuzi na ueledi  katika kuwahudumia wateja na kuongeza tija katika kutekeleza majukumu mbalimbali Pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji katika utendaji kazi.


Katika mafunzo hayo yaliyoendeshwa na Afisa Utumishi Mkuu ndugu Protace T Magayane , yalilenga kuwapitisha watumishi hao katika mada mbalimbali ikiwa ni pamoja na Utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia muundo, Maana na umuhimu wa OPRAS, Mawasiliano thabiti ya Mtumishi wa Umma kwenye Taasisi, Mavazi ya staha kwa Mtumishi wa Umma, Elimu ya magonjwa ya dharura, Maadii ya wa Mtumishi wa Umma, Uandaaji wa mihtasari mbalimbali, Utendaji kazi kwa pamoja (Team Work), Dhana YA 5S KAIZEN, Dhana ya kutembea pamoja, Matumizi bora ya Mifumo  na vifaa vya TEHAMA serikalini, Umuhimu wa utunzaji wa takwimu, Namna ya kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya mripuko mf Corona na Uandaaji wa ripoti mbalimbali.


Mwezeshaji,  Afisa Utumishi Mkuu, Ndugu Protace T.  Mgayane akiwapitisha watumishi kwenye mada mbalimbali  wakati wa mafunzo ya watumishi wapya 

katibu wa Afya Bi Getrude Mhimbi akiwapitisha washiriki wa mafunzo katika mada ya Utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia muundo.

watumiishi wapya wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizowasilishwa  katika mafunzo yao

Mafunzo hayo yalifungwa na Daktari Bingwa macho Dkt Juma Katwale na kuwaeleza washiriki wote kuzingatia mambo yote waliyoyapata katika mafunzo hayo

picha: Dkt Juma Katwale akifunga mafunzo ya watumishi wapya

picha ya pamoja ya watumishi wapya pamoja na wawezeshaji wa mafunzo hayo