Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu
(Simiyurrh)

Makabidhiano ya Hospitali ya Rufaa Simiyu

Posted on: November 17th, 2019
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu ndugu Jumannne Sagini amefanya makabidhiano ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa simiyu kwenda kwa Katibu Mkuu Afya katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu tarehe 18/11/2019


Makabidhiano hayo yalihusisha utiaji saini wa nyaraka za makabidhiano ambapo Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Simiyu Dr Matoke Muyenjwa alimuwakilisha Katibu Mkuu- Afya.

Jambo  hili kisheria limefanyika mbele ya viongozi mbalimbali wa serikali, Timu ya uendeshaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu, mwakiliishi toka wizara ya fedha, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bodi ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, timu ya uendeshaji wa shughuli za afya Mkoa na viongozi toka Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi

Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dkt. Matoke Muyenjwa alisema kuwa Makabidhiano hayo sio mwisho wa ushirikiano kwani wataendelea kufanya kazi kwa Pamoja kama ilivyo Kauli mbiu ya Wizara  ya Afya  "Tutetembee pamoja' na aliendelea kwa kutoa shukurani kwa  viongozi wa Mkoa hususani Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Mh Sagini kwa  kuongeza  eneo la ekari 18 katika eneo la Hospitali  na kulifanya eneo hilo kuwa na jumla ya ekari 80 na kumpongeza  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji kukubali kupima eneo hilo kwa  haraka

"Nawapongeza wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu kwa namna wanavyohudumia wagonjwa, wakati mwingine huwa napita usiku kwa kuwa ni karibu na ninapoishi, lakini attension ya vijana wale katika kuhudumia wagonjwa iko vizuri sana na nawasihi waendelee na moyo huo kwa masirahi mapana ya nchi yetu " alisema Mhe. Jumanne Sagini

"Kwa vituo  vyetu vyote tulivyojenga tumeviwezesha na kuwafundisha watumishi, na hivyo Wafanyakazi wazembe wachukuliwe hatua ili  iwe fundisho kwa wengine.Hospitali ya Somanda malalamiko ni mengi lazima kufanyike mabadiliko, watumishi wabadilike watakaokaidi hatua  kali zitachukuliwa dhidi yao, Hatutaki watumishi wa Afya waingiliwe katika majukumu yao, ila watoe huduma kama walivyofundishwa na wazingatie viapo vyao .Watumishi wawe  Wabunifu ikiwezekana waweke 'FAST TRACK' kwani Wapo Watanzania ambao wapo tayari kulipia huduma bora. Watumishi wayapende Maeneo wanayofanyia kazi, wayatunze na  kuyafanyia ukarabati utakaodumisha na kuboresha mazingira.Vituo vya Somanda na ikindilo vinatakiwa vifanye mabadiliko katika utendaji kazi wao" Alisema  Mh Jumanne Sagini

 Mjumbe wa bodi ya Hospitali ya Rufaa alimalizia kwa kutoa Shukurani kwa Mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala katika kutekeleza jukumu la makabidhiano na kuahaidi kuendelea kutoa ushirikiano katika kutoa huduma za afya Mkoani Simiyu.