Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Simiyu
(Simiyurrh)

UPANDAJI WA MITI YA KIVULI NA MATUNDA HOSPITALI YA MKOA WA SIMIYU WALETA MADHARI YA KUVUTIA

Posted on: November 20th, 2019

Wafanya kazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa wa Simiyu wameshiriki  katika zoezi la upandaji wa miti ya kivuli na matunda katika eneo la mazingira ya Hospitali. Zoezi hililimefanyika leo tarehe 25/11/2019 likiongozwa na Afisa Afya Mazingira wa Hospitali Bi Glory Stanley Mndasha

Bi Glory aliendelea kwa kusema kuwa miti huchangia kwa kiasi kikubwa katika upatikanaji  wa mvua ambayo ina umuhimu mkubwa katika Maisha yetu ya kila siku kwa kutupatia Maji safi na kukuza mazao mashambani. Ukosefu wa mvua kwa muda mrefu hupelekea  Ukame na Baa la Njaa katika jamii . Miti hutunza vyanzo vya maji. huleta hewa safi ya oksijeni na husaidia kupunguza Kabonidaioksaidi(hewa ukaa) kutoka katika Mazingizra tunayoishi. Pia miti hutoa Madawa mbalimbali yanayotumika Kutibu Magonjwa mbalimbali,na husaidia sana katika kukinga upepo,Na hivyo huepusha athari zaidi ya Upepo mkali. Pamoja na hayo miti Huifanya ardhi ishikamane na hivyo kuzuia mmomonyoko wa udongo. MIti ya matunda hutupatia chakula (matunda) ambayo hutumiwa na binadamu pamoja na wanyama wengine

"Tumepanda miti 60 ya matunda ambayo ni mchanganyiko wa miembe, miparachichi na michungwa  na miti 50 ya kivuli  pamoja na maua mbalimbali kuzunguka eneo la Hospitali, Ni vyema kutumia kipindi hiki cha mvua katika kupanda miti ili iweze kustawi vizuri kwa kupata maji ya kutosha, hatua hii muhimu itasaidia katika kutunza mazingira yetu" Alisema Bi Glory  Mndasha

wafanya kazi wa SUMA -JKT wakisaidia zoezi la upandaji miti

Afisa Afya Mazingira wa Hospitali Bi Glory Stanley Mndasha akitekeleza zoezi la upandaji miti